Wamesema kushiriki
kwako katika vikao hivyo kutasaidia sana katika kuhakikisha kwamba, wale wanaopata
msamaha huo hawatojihusisha tena na
vitendo vya uhalifu warudipo uraiani.
Ombi hilo limetolewa
na Mkuu
wa Upelelezi Mkoa wa Rukwa Kamishna Msaidizi wa Polisi Ralph Meela,
wakati alipopewa fursa ya kutoa
tathimini yake kuhusu hali ya utoaji hakijinai katika mkoa wa
Rukwa, mafanikio na changamoto wanazokabiliana
nazo.
Ilikuwa katika kikao cha pamoja kati ya Makatibu Wakuu watatu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi
ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora na Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto na Wadau wa vyombo vya utoaji haki, kikao kilichofanyika leo (
Alhamisi) katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
“ Tunashukuru sana kwa ujio wenu katika Mkoa wa Rukwa, hali ya utoaji Hakijinai kwa mkoa wetu kwa
kweli ni nzuri. Ila ningependa nigusie katika kipengele cha msamaha wa wafungwa. Tungeomba na sisi wadau
wa upelelezi katika Jeshi la Polisi na wadau wengine tushirikishwe katika vikao
vya uchambuzi” akaomba Mkuu wa Upelelezi
Mkoa wa Rukwa.
Amebanisha kwamba, kwa
kushiriki vikao vya uchambuzi kunaweza
kusaidia katika kutoa mchango wa mawazo na maoni yao yatakayosaidia kubainisha
ni mfungwa gani kweli anastahili kupata msamaha na hata akirudi uraiani hata
leta matatizo
“Katika mkoa wetu wafungwa 58 walipasa msamaha wa Rais,
lakini wiki moja baadaye wawili kati yao walikamatwa kwa makoa ya kuiba mbuzi na mwingine kuvunja duka. Kama wapelelezi wangeshirikishwa katika
vikao uchambuzi pengine hawa wawili
wasingestahili kupata msahama kwa sababu
tunafahamu mienendo ya wafungwa wengi”akasisitiza
Akichangia kipengele
hicho cha msamaha wa wafungwa, Mrakibu wa Magereza Mkoa wa Rukwa SP Daniel
Ndamgilire yeye alieleza kuwa linatakiwa jopo la madaktari watano watakaowafanyia
uchunguzi wafungwa ili kubaini wale
wanaostahili kupata msamaha jambo ambalo amesema linachangamoto kubwa katika
kulitekeleza.
“ Na mimi nichangie kidogo katika kipengele hiki cha msamaha
wa Rais, kunatakiwa uwepo wa jopo la madaktari watano, kwa mfano
anatakiwa awepo daktari wa kuwapima wazee,
daktari wa watoto, daktari wa wamama wajawazito, na wengineo, hii ni changamoto
kubwa kwetu kuwapata madaktari wote hao kwa wakati mmoja, tunaomba hili nalo
liangaliwe” akasema SP Ndamgilire
Katika hatua nyingine
Mkoa wa Rukwa umetoa mapendekezo
kadhaa yatakayosaidia kuboresha utoaji
haki katika Mkoa huo.
Baadhi ya mapendekezo hayo ni kupewa kipaumbela kwa
ujenzi wa gereza na mahabusu ya watoto
wakati wa ujenzi wa miundombinu ya vyombo vya kutoa
haki.
“Mkoa wetu katika ujenzi wa miundombinu ya vyombo vya utoaji
haki unapendekeza gereza na mahabusu ya watoto ipewe kipaumbele wakati ya
ujenzi huo ili kuwasaidia na kuwaepusha watoto wanaokinzana na sheria wasipelekwe
magereza ya watu wakubwa” imesema Taarifa ya Mkoa iliyosomwa na Wakili Frida
Hava.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uwepo wa gereza na mahabusu ya
watoto siyo tu kutawaepusha watoto hao
kujinfuza mbinu zaidi za kufanya uhalifu lakini pia kutawaepusha kufanyiwa
vitendo vya kikatili.
Pendekezo hilo la
kuwapo kwa gereza na mahabusu za
watato liliungwa mkono pia na Mama
Varelia ambaye ni mmoja wa waratibu
wa Kamati za ulinzi wa wanawake na watoto (MTAKUWA)
alisema kutowekuwapo kwa gereza na mahabusu ya watoto mkoani humo kunawaweka watoto katika mazingira hatarishi.
“Hata sasa hivi ukiendea pale
gerezani utakuta watoto wamewekwa
koridoni kwa sababu hawawezi kuchangwa na wafungwa wengine, wanaishi
katika mazingira magumu sana, nisisitize na mimi ujengi wa gereza na mahabusu ya watoto katika
mkoa wetu upewe kipaumbele,
Wakati huo huo wadau hao wa Hakijinai katika Mkoa wa Rukwa
wametoa pendekezo kwa Serikali
la marekebisho ya Sheria
zinazochelesha mtuhumumiwa kupata haki yake yafanyike mapema.
Mfano wa Sheria wanayoshauri ifanyiwe marekebisho ya mapema
ni Sheria inayomtaka binti aliyepata
ujauzito kusubiri hadi ajifungue ndipo
vinasaba vya mtoto ( DNA) viende
kulinganishwa na mtuhumiwa.
Wamesema Sheria hii inaleta mkanganyiko ambao ni pamoja na
watuhumiwa na mashahidi kutopatikana tena na au tatizo hili kumalizwa kimila au
kifamilia jambo ambalo wanasema linachangia
kumyima haki Binti.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...