Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 umezindua mradi wa zahanati katika kijiji cha Mabalanga wilayani Kilindi Mkoani Tanga.

Akisoma risala mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge, Mganga Mkuu wa Wilaya ya kilindi, DMO Daniel Chochole amesema mradi huo utakapokamilika utahudumia wananchi wakazi zaidi wa Kijiji hicho pamoja na Vijiji jirani.

Kwa upande wake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka huu, Josephine Mwambashi amesema baada ya kuukagua mradi huo ameridhika kwa sababu thamani ya fedha za ujenzi inalingana na uhalisia.

Kwa kuonyesha kuridhirika na mradi huo,Kiongozi huyo aliwaongoza wenzake kusafisha kiwanja kitakachojengwa nyumba ya daktari kwa wa zahanati hiyo nguvu za wanananchi.

Wakazi wa Kijiji cha Mabalanga ambao sehemu kubwa ya mradi huo umechangiwa na nguvu zao wamesema wanaisubiri kwa hamu zahanati hiyo kwa sababu wanapougua wamekuwa wakitembea umbali mkubwa kufuata tiba.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya kilindi, DMO Daniel Chochole

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...