Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ameshusha neema kwa wananchi wa Kilosa kwa uamuzi wa kufuta jumla ya mashamba 11 yenye ukubwa wa ekari 24,119 katika wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro na kugawiwa kwa wananchi kwa ajili ya shughuli za kilimo, ufugaji na uwekezaji.
Aidha,
Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia ufufuaji wa mashamba 49 yenye ukubwa
wa ekari 45,788.5 yaliyotaifishwa miaka ya nyuma huku na wananchi
wakiwa hawana uhakika nayo ambapo Mhe. Rais ameelekeza sehemu kubwa ya
mashamba hayo kutumiwa na wananchi kwa shughuli za kilimo.
Uamuzi
huo wa Rais Samia Suluhu Hassan unetangazwa leo tarehe 7 Juni 2021
wilayani Kilosa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William
Lukuvi akizungumza kwa nyakati tofati na viongozi, watendaji na
wananchi wa kijiji cha Kimamba wilayani Kilosa wakati wa ziara yake
mkoani Morogoro.
Hata
hivyo, Waziri Lukuvi alisema pamoja na kufutwa mashamba hayo
haimaanishi kama yako huru kwa kila mtu kujichukulia bila utaratibu na
timu maalum imeundwa kwa ajili ya kupanga matumizi ya ardhi katika
mashamba hayo na kutahadharisha asitokee mtu yeyote kuzuia timu hiyo
kufanya kazi yake.
Naye
Mbunge wa jimbo la Kilosa ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria
Profesa Palamagamba Kabudi mbali na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan
kwa maamuzi aliyoyachukua kufuta mashamba 11 na kuridhia sehemu kutolewa
kwa wananchi, alisema uamuzi uliofanywa na Rais unawagusa wana Kilosa
hasa wana Kimamba na kuwataka kumuumga mkono kwa juhudi anazofanya
kuwatumikia wananchi.
Baadhi
ya mashamba yaliyofutwa ni pamoja na Sumagro Ltd lililopo Madoto na
lenye ukubwa wa ekari 7,712, Bumagro Ltd Kivungu ekari 5660, M/S Sino
Development (T) Ltd lililopo Kimamba ekari 6,945, Abdalah Islam lililopo
eneo la Dodoma Isanga ekari 307, Mifugo Magairo la Magole lenye ukubwa
wa ekari 489 na shamba la MS Masoni Company lililopo Magole ekari 466.
Mengine
ni Mitibora (T) Ltd ekari 511 eneo la Magoli, Abdalah Islam ekari 307
Isanga Dodoma na Ibrahim Magairo mwenye shamba lenye ukubwa wa ekari 516
lililopo eneo la Magole.
Katika
mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya mashamba 123 yalihakikiwa katika
wilaya za Kilosa, Mvomero na Morogoro DC na kati yake mashamba 11 yenye
ukubwa wa ekari 24,119 yalibatilishwa na Mhe. Rais kutokana wamiliki
wake kukiuka taratibu za uendelezaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...