Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania
JWTZ Luteni Jenerali Yakoub Mohamed
Jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania JWTZ kwa
kushirikiana na Jeshi la Marekani wanatarajia kufanya Mafunzo Maalum
kukabiliana na Vitendo vya Uhalifu ikiwemo Ugaidi.
Hafla
ya Kufungua Mafunzo hayo umefanyika leo Julai 28 katika kituo cha
Ulinzi wa Amani na Mkuu wa Kamandi ya Afrika wa Jeshi la Marekani
Jenerali Stephen Townsend Kunduchi Dar es Salaam.
Jenerali
Toensend amesema Tanzania na Marekani zimekua na ushirikiano katika
mambo mbalimbali hivyo ni sehemu sahihi katika Mafunzo hayo
maalumu.
Kwa
Upande wake Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania
JWTZ Luteni Jenerali Yakoub Mohamed amesema jeshi la Marekani limekua
likishirikiana vyema na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika Mafunzo
mbalimbali
Mafunzo
Hayo maalumu ya Mwezi mmoja kwa ajili ya Kukomesha Vitendo vya Uhalifu
ikiwemo, Ugaidi na vitendo vingine kama hivyo ambavyo vimekua
vikitokea katika Mataifa Mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...