Ujenzi wa Daraja katika Mto Mayugu katika eneo la Kabunde linalojengwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe , Mkoani Katavi kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) litakalogharimu zaidi ya shilingi milioni 112 kwa kutumia fedha za mfuko wa barabara katika bajeti ya fedha ya mwaka 2020/2021
lengo la kufungua daraja hilo ni kunusuru adha ya wananchi kuvuka kwenye maji katika eneo hili wakati wa mvua . Pia kutoa huduma za usafiri na usafirishaji wa mazao ya wakulima kutoka shambani kwenda sokon.
Daraja hilo likikamilika linategemewa kutoa huduma kwa wananchi zaidi ya watu 91,313 na kuwahudumia wakulima zaidi 12,692 kwa ajili ya kusafirisha mazao kwenda maeneo mbalimbali kujipatia riziki.
Home
HABARI
UJENZI WA DARAJA MTO MAYUNGU MKOANI KATAVI LITAONDOA ADHA KUBWA YA WANANCHI KUSAFIRI KWENYE MAJI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...