Manispaa
ya Lindi iliongezewa eneo la Utawala kutoka Halmashauri ya Wilaya ya
Lindi (Lindi DC) ambalo liliangukia kwenye Jimbo la Mchinga na Kamati ya
Fedha na Utawala kwenye kikao Maalumu cha Tarehe 05/06/2020 walijadili
na kupokea mali,bajeti na watumishi wa iliyokuwa sehemu ya Lindi DC
(Jimbo la Mchinga)
Kikao hicho kwa kauli moja
walikubaliana kuhamishiwa sehemu ya bajeti ya 2020/21 ya eneo la
Mchinga kwenye Manispaa ya Lindi na kufanya ukomo wa bajeti ya Manispaa
hiyo kuongezeka kwa Shilingi Bilioni 1,059,227,980 na kiasi hicho hicho
kupungua kwenye ukomo wa bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Lindi ambapo
kwa sasa inajulikana kama Halmashauri ya Wilaya ya Mtama.
Baada
ya ongezeko hilo kwenye ukomo wa Bajeti ya Manispaa ya Lindi ilifikia
kiasi cha Shilingi Bilioni 3,500,834,000 badala ya ile ya awali ya
Shilingi Bilioni 2,443,320,000.
Hivyo, Taarifa
iliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mhe. Ummy
Mwalimu ilijielekeza kwenye mabadiliko yaliyofanyika ya kuhamishiwa kwa
eneo hilo la utawala na mali zake, ambapo hadi kufikia Juni 30, 2021,
Manispaa ya Lindi imekusanya kwa asilimia 58% ya ukomo wa bajeti ya
Shilingi Bilioni 3,500,834,000.
Hata hivyo,
Baraza la Halmashauri ya Manispaa ya Lindi wamejielekeza kwenye Bajeti
ya awali kabla ya kuongezewa eneo la utawala ambayo ni Shilingi Bilioni
2,443,330,000 bila kuzingatia mabadiliko yaliyofanywa.
Kufuatia
hali hii, Mhe.Waziri Ummy anawahimiza madiwani na watendaji wa
Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kuongeza jitihada za ukusanyaji wa
mapato ya ndani ya Manispaa hiyo ili kuweza kutoa huduma bora za jamii
kwa wakazi wa manispaa hiyo ikiwemo kutekeleza miradi ya maendeleo ya
wananchi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mhe. Ummy
Mwalimu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...