Na Zainab Nyamka, Michuzi TV


WABUNGE wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wameipongeza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar Es Salaam (DAWASA) kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.

Kwa sasa Dawasa inatoa huduma kwa asilimia 92 kwa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani na wakitumia takribani Bilioni 50.4 kwa mwaka katika kuboresha huduma za maji.

 Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameweza kuzindua Cheti cha Ubora ISO na magari ya kutolea majitaka yatakayotumika kuboresha huduma ya majitaka ndani ya Jiji la Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa wakati wa hafla iliyoandaliwa na Mamlaka hiyo leo Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wabunge wa Mikoa inayohudumiwa nayo na kuwashukuru Dawasa kwa kufanikisha miradi mikubwa na kuondoa changamoto ya maji kwenye maeneo yaliyokuwa hayana huduma.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mbunge wa Ilala Mussa Zungu amempongeza Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Cyprian Luhemeja kwa kuisimamia vizuri Mamlaka hiyo na kufikia malengo waliyojiwekea na 

Zungu amesema, Kwa upande wa Wilaya ya Ilala changamoto kubwa ni upande wa majitaka ambapo ameona leo uzinduzi wa magari ya majitaka na hilo linaenda kuchagiza uboreshaji wa huduma ya majitaka na amemsikia Mhandisi Luhemeja akielezea mkakati wa ujenzi wa miradi mikubwa ya majitaka.

Mbunge wa Jimbo la Ukonga Jerry Silaa, amemshukuru mtendaji mkuu pamoja na watendaji wote wa Dawasa kwa kufanikisha maji kufika katika jimbo lake ikiwa ni miaka mingi wakiwa hawapati majisafi na Salama.

Silaa amesema, watendaji wote wanafanya kazi kubwa sana na wananchi wa Ukonga wanapata maji yakiwa yamefika kwa uhakika wakitumia tanki la Pugu ambalo lilizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Hassan Suluhu.

Naye Mbunge wa Segerea, Bonna Kamoli amesema dawasa wanatenda haki ushahidi huo anao kwa sababu katika Jimbo lake hakukuwa na maji ila sasa wananchi wake wameanza  kupata maji safi na miradi mingine ya kimkakati ikiendelea kujengwa.

Wabunge wengine waliohudhuria ni Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete, Hawa  Mchafu, Subira Mgalu, Abdalla Chaurembo, Mbunge wa Kibamba Mtevu na Mbunge wa Bagamoyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akipokea tuzo kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange wakati w hafla ya tathmini ya utendaji kazi.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...