Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

Wakazi wa Kigamboni na Mkuranga kuondokana na kero ya maji mara baada ya kumalizika unategemea kukamilika mwaka 2022. Hii ni kutokana na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (DAWASA) kutenga fedha kwa ajili ya miradi hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara ya kumaliza ziara hiyo, Naibu Waziri, Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema serikali iko makini hasa kwenye kusimamia miradi ya maji ili kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo mbalimbali ya hapa nchini.

Pia amempongeza Afisa Mtendaji Mkuu, Cyprian Luhemeja kwa kuwapa nafasi wafanyakazi waliochini yake ili kuonesha uwezo mkubwa wa kazi na hii inajidhiirisha kwamba wameweza kuonesha umahili hasa kwenye kusimamia miradi mbalimbali ya DAWASA ambayo ni mikubwa kwa kushirikisha wataalamu wa ndani wakiwemo wa Wizara ya Maji pamoja na  na wakandarasi wageni ili kupelekea kupata ujuzi zaidi.

Amesema kutokana na kutumia wataalam wa ndani hasa wakandarasi wataweza kubaki na ujuzi hivyo wataweza kusimamia miradi mingine inayokuja ili kuwainua zaidi na kupelekea kupunguza gharama kwa kutumia wakandarasi wazawa ili kuweza kuwafikishia huduma ya maji wananchi.

Pia amewapongeza DAWASA kwa kutoa nafasi kubwa kwa wanawake na kupelea kufanikisha miradi mbalimbali hivyo ametoa wito kwa taasisi mbalimbali kuiga mfano wa Mamlaka hiyo kuwaamini wanawake kwani wanaweza kufanya kazi kiufanisi na bila shida yoyote maana hawahitaji kuona mwanamke anapendelewa ila apimwe uwezo wake ili kuwa na wataalam wazuri.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA, Mhandisi Ramadhani Mtindasi mradi wa Kisarawe II utakaosaidia kuondoa kero ya Maji katika Kata saba za  wilaya ya Kigamboni  kutokana na kuchimba visima katika eneo la Kigamboni na kujenga tenki la maji litakalokuwa linaweza kuhifadhi maji lita Milioni 15.

Pia amesema Mradi wa Mkuranga – Vikindu umeweza kupunguza kero ya maji hasa maeneo ya Mkuranga hivyo mradi huo ukimalizika utaweza kuondoakero ya maji mara baada ya kujenga tanki la maji linalohifadhi maji lita milioni 1.5.

Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akipokea taarifa kuhusu mradi wa maji wa Kigamboni utakavyoweza kuhudumia kata 7 za Kigamboni wakati wa ziara yake iliyofanyika Kigamboni na Mkuranga.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kuhusu tenki linalojengwa katika eneo la Kigamboni litakalokuwa na ujazo wa maji Milioni 15 mara baada ya kutembea ujenzi wa tanki hilo.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi akiwatambulisha wafanyakazi wa DAWASA pamoja na wakandarasi wa mradi wa Kisarawe II kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi mara baada ya kuwasili ili kukagua mradi wa maji wa Kigamboni utakavyoweza kuhudumia kata 7 za Kigamboni wakati wa ziara yake iliyofanyika Kigamboni unaotekelezwa na DAWASA.
 Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akikagua ujenzi wa tenki la kuhufadhia maji litakalokuwa  na ujazo wa milioni 15 za maji kutoka kwenye visima mbalimbali vilivyochimbwa katika Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam.
Muonekano wa tenki la maji linalojengwa na DAWASA katika kata ya Kisarawe II litakalokuwa na ujazo wa milioni 15 za maji na kumaliza hadha ya maji katika kata zote Saba za Kigamboni.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi kuhusu moja ya kisima chenye urefu mita 603.5 kwenda chini kilichopo katika kata ya Kisarawe II katika Wilaya ya Kigamboni wakati wa Ziara yake ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akipata maelezo kutoka kwa Mkandarasi wa mradi wa Kisarawe II Mehrdad Talebi(wa kwanza kulia) kuhusu namna walivyoweza kwenda kwa wakati kwenye uchimbaji wa visima hivyo pamoja na ubora wa maji ya visima hivyo alipotembelea moja ya kisima chenye urefu mita 603.5 kwenda chini kilichopo katika kata ya Kisarawe II Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akizungumza na viongozi wa DAWASA pamoja na mkandarasi wa mradi wa Kisarawe II mara baada ya kumaliza  akikagua ujenzi wa tenki la kuhufadhia maji litakalokuwa na ujazo wa milioni 15 na moja ya kisima chenye urefu mita 603.5 kwenda chini kilichopo katika kata ya Kisarawe II Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi  akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi( wa kwanza kulia)  kuhusu kituo cha kusukumia maji kilichopo Mkuranga mkoani Pwani Wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akikagua kituo cha kusukumia maji kilichopo Mkuranga mkoani Pwani Wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi( wa kwanza kulia) kuhusu namna kituo cha kusukumia maji hicho kinavyofanya kazi kilicakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Muonekano wa pampu ya kusukumia maji iliyopo Mkuranga Mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi( wa kwanza kulia) kuhusu namna ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa Lita Milioni 1.5 ulivyofanyika pamoja na linavyowahudumia wakazi wa Mkuranga ziara yake ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa na DAWASA.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mtindasi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna walivyoweza kutekeleza miradi ya Kisarawe II pamoja na Mkuranga-Vikindu kwa kutumia asilimia 35 ya Mapato yanayokusanywa na DAWASA na kwenda kwenye miradi wakati wa Ziara ya Naibu Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi alipokuwa anakagua miradi inayotekelezwa na DAWASA.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara yake kwenye miradi Kisarawe II pamoja na Mkuranga-Vikindu na kujionea ufanisi wa miradi hiyo inayotekelezwa na DAWASA.
Muonekano wa tanki la maji la Mkuranga lenye uwezo wa kujaza maji Lita Milioni 1.5 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...