Na Zainab Nyamka, Michuzi TV
"YANGA IS BACK", Ni maneno ya Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Al Nabi baada ya kuangalia kiwango cha wachezaji wake na kuondoka na alama tatu muhimu katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ilifaniiwa kupata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya watani zao wa jadi Simba katika mchezo uliochezwa jana kwene dinmba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kocha Nasreddine amesema anafurahishwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake katika dakika zote 90 na kufanikiwa kupata ushindi huo kutoka kwa wapinzani wake Simba,
Amesema, mchezo ulikua mzuri sana na Simba ni timu nzuri waliingia uwanjani wakiwa wamejipanga kuhakikisha hawaruhusu kufungwa na hilo limefanikiwa baada ya wachezaji wake kuonesha nidhamu kubwa sana.
"Simba naijua ni timu nzuri, na tuliingia kwa tahadari kuhakikisha haturuhusu Simba kuutawala mchezo huo na wachezaji wangu walifuata maelekezo, nimefurahi sana kupata ushindi huu,"amesema Nasreddine
Ameeleza, ushindi wa jana dhidi ya Simba ni ishara kuwa sasa timu yake imeanza kurejea katika kiwango chake na ligi na palipo na mapungufu atafanyika kazi.
Nasreddine ameongezea na kusema kwa sasa wanajiandaa na michezo miwili iliyosalia wakiwa na alama 70 nyuma ya Simba walio na alama 73 wakisalia na michezo minne.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...