Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge,leo Agosti 7,2021 ameshiriki Mazishi ya Watoto watano waliofikwa na mauti kwenye Ajali iliyohusisha Pikipiki na Fuso Eneo la  Kata ya Kimange Halmashauri ya  Chalinze.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Wankyo Nyigesa  Ameeleza kuwa Mnamo Tarehe 6 Agosti, 2021 majira ya saa 1 :15 Jioni  Gari aina Mitusubish Fuso Na 198 CWN ikitokea Dar es salaam kwenda Arusha iligonga  Mwendesha Pikipiki  kusababisha vifo vya Wanafunzi wanne pale pale na mmoja kufariki akipatiwa matibabu Hospital ya Jeshi Kihangaiko.

Ameeleza kuwa Wanafunzi hao watano wa Kimange Sekondari  walikuwa wamepakiana kwenye Pikipiki wakitokea  Kimange kuelekea Mbwewe. Wanafunzi hao walikuwa wakitokea michezoni shule Jirani ya kwamakocho Sekondari.

Wanafunzi hao waliofariki ni  Laya Ubwa  Masudi (16) mwanafunzi wa kimange Sekondari Kidato cha tatu,  Furaha Athumani (16) Mwanafunzi Kimange Sekondari Kidato cha tatu, Athumani Bushiri (15) Mwanafunzi kimange Sekondari Kidato cha Kwanza, Amina Msomba (15) Mwanafunzi Kimange Sekondari Kidato cha Kwanza na Athumani Mchafu (17) Mwanafunzi Kidato cha tatu.


Ameeleza kuwa Chanzo cha Ajali hiyo ni Uzembe wa Dereva wa  Gari na mwendo kasi uliosababisha kushindwa kumudu Gari hilo na kupelekea kumgonga  Mwendesha Pikipiki akiyekuwa mbele yake.

Amethibitisha kuwa Jeshi la polisi limefanikiwa kumshikilia Dereva wa Gari hilo kwa ajili ya hatua za kisheria,

Kunenge ametoa pole sana kwa Familia na Wananchi wa Kata hiyo kwa Msiba Mkubwa ambao wameupata. "Kwa niaba ya Mhe Rais Mhe. samia Suluhu Hassan nitoe pole  nyingi kwenu alisema Kunenge" "Kubwa zaidi kwetu ilikuwa ni kuja kushiriki nanyi, tumekuja na Swadaka Ndogo kwa ajili ya kufariji familia hizi.

"Yaliyotokea yametokea, niwaombe tuzingatia matumizi ya vyombo vya Moto. Sisi kwa upande wa Serikali tunaendelea kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria za Nchi. Dereva wa Gari hilo tunaye tutachukua hatua" Alisema Kunenge.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...