Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga mwishoni mwa wiki amekagua utendaji wa Sekta ya Maji mkoani Mtwara.

Mhandisi Sanga katika ziara hiyo ya kikazi amewataka watendaji na wataalamu wa sekta ya maji kutumia ubunifu katika kutoa huduma, na kuepuka gharama ambazo hazina ulazima.

Amesisitiza wataalamu kutumia usanifu wa miradi utakaowezesha majisafi kuwafikia wananchi kwa njia ya mserereko, hivyo huduma hiyo kumfikia mlaji kwa gharama ndogo.

Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga akikagua chanzo cha maji cha Mbwinji kinachotumiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Masasi Nachingwea (MANAWASA) kusambaza huduma ya maji, (kulia) ni Mkurugenzi Mtendaji wa MANAWASA Mhandisi Nuntufye Mwamsojo.

Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga akitoa maelekezo ya kitaalamu kuhusu ujenzi unaoendelea wa mradi wa maji wa Chipingu, pamoja naye (katikati) ni Mbunge wa  Lulindi Mhe. Issa Ally (Mb) na wataalamu wa sekta ya maji. Chanzo cha maji cha mradi huo ni mto Ruvuma.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...