Na Sixmund J. Begashe.
 
Makumbusho ya Taifa la Tanzania imepokea ugeni wa Uongozi na Wataalam wa Makumbusho ya Taifa ya nchi ya Malawi ambao utakuwa nchini kwa siku sita ili kupata uzoefu wa namna ya uendeshaji wa shughuli za kimakumbusho.

Akiwapokea wageni hao katika uwanja wa ndege wa Mwl Nyeyere Dar es Salaam, Mratibu wa program ya wageni hao wa Makumbusho ya Taifa nchini, Bi Frida Kombe amesema ni faraja kubwa kuona nchi za nje zinaiona Tanzania kama Mwalimu wa uhifadhi wa Urithi wa Utamaduni na Malikale.

Wakiwa nchini, licha ya kujifunza shughuli za uhifadhi pia siku ya Ijumaa tarehe 24 September 2021 watapata nafasi ya kutanzama maonesho ya Museum Art Explosion, kufanya Utalii katika jiji la Dar es Salaam (Dar City Tour) na Bagamoyo Mkoani Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...