Na Linda Shebby, Kibaha
MKUU wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge amesema katika kuhakikisha wanafikia lengo la utoaji wa chanjo ya Uviko 19 , chanjo hiyo itakua ikitolewa nyumba kwa nyumba.

Mkuu huyo wa Mkoa aliyasema hayo  leo Kibaha Mkoani Pwani  alipokuwa katika ufunguzi wa semina ya Afya  ya Msingi ya Mkoa  kuhusu chanjo dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19 ambapo semina  hiyo imewahusisha  wakuu wa  Wilaya  zote kutoka Mkoani Pwani , Kamati ya Ulinzi na Usalama , viongozi wa dini na wadau mbalimbali wa afya Mkoani hapa

Akizungumzia  kuhusu muitikio wa  utoaji chanjo  hiyo   ya Uviko  19 Mkoani Pwani alisema kuwa  hadi sasa  Mkoa umefikia nusu ya lengo ambapo hali halisi ya waliochanja  hadi  sasa ni asilimia 50  huku chanjo   zilizotolewa  30,000  na achanjo ambazo bado hazijatumika  ni 15, 000  kwa Mkoa wa Pwani  huku  Wilaya mbili za Bagamoyo na Kibaha Mji ndiyo wameongoza kwa muamko wa  kupata chanjo hizo.

"Pwani tumejiwekea mpango mkakati wa utoaji chanjo  hizi za Uviko 19  ambapo tutawafikia wananchi katika maeneo mbalimbali ya mikusanyiko,tutapita nyumba kwanyumba ikiwemo kwenye mihadhara ya kidini na makongamano  mbalimbali ambapo wengi hupatiwa elimu baada ya kufahamu  vizuri faida  ya chanjo  hizi huridhia kuchanja baada ya kupatiwa  taarifa sahihi jinsi chanjo hiyo inavyoweza  muhusika aliyechanjwa " alisema  Kunenge.

RC Kunenge alisema kuwa serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ina njema kwa kutoa chanjo hizo kwa wananchi wake  huku akisisitiza chanjo   ya Uviko 19 liyobaki  ikatumike  kwa kuwachanja wananchi Ili kuinusuru isiweze kuharibika.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa  Pwani Dokta Gunini  Kamba ametoa wito kwa vijana wenye umri  kuanzia   miaka 18 hadi 45 kuachana na  mawazo potofu kwamba ugonjwa huu hauwadhuru sana  vijana kutokana na umri wao mdogo huku akisisitiza kwamba ni muhimu wajitokeze kupata chanjo hiyo itasaidia  kuongezea  kninga zao za mwili huku akisisitiza kwamba chanjo hizi hazina madhara yeyote   kama jinsi inavyo vumishwa na wachache wenye  nia ovu.
Dokta Gunini aliongeza kwa kusema kuwa wataahirikiana katika ngazi zote  Ili kuhakikisha wanafikia lengo la kutoa chanjo hizo za Uviko 19.

Dokta Gunini aliongeza kwa kusema kuwa  utaratibu huu wa kutoa elimu juu ya umuhimu kupata  chanjo ya Uviko 19  wameanza nayo tangu walipoanza   kutoa chanjo  hiyo Mkoani Pwani ambapo wamekua wakitoka elimu  kwa wananchi na wadau mbalimbali ikiwemo katika masoko na sehemu mbalimbali zenye mikusanyiko.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...