NA TIGANYA VINCENT

HALMASHAURI ya Wilaya ya Uyui imetuma barua ya pongeza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia kiasi cha shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa vyumba 123 vya madarasa kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano ya UVIKO 19 .

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Said Ntahondi kwa niaba wenzake ameikabidhi barua hiyo leo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani kwa ajili ya kumfikishia Rais Samia.

Alisema kwa kipindi kifupi cha uongozi wa Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia , Uyui imepata fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara.

Alisema kati ya fedha hizo shilingi bilioni 2.4 ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Sekondari na bilioni 1.1 kwa ajili ya vyumba vya madarasa katika Shule Shikizi.

Ntahondi alisema kuwa kiasi cha shilingi milioni 90 ni za ujenzi wa watumishi wa sekta ya afya na milioni 14.1 kwa ajili ya fedha za ufuatiliaji.

Alisema watahakikisha watumia kiasi cha milioni 20 kukamilisha darasa moja kama walivyoekelezwa na kiasi kibaki .

Ntahondi aliongeza hivi Madiwani na Watendaji wa Halmashauri hiyo wamejipanga kusimamia ili kuhakikisha fedha zinatumika kwa makusudio yalipangwa.

Aidha Mwenyekiti huyo alisema aliwafanyia Rais Samia ameshamaliza kazi


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui  Said Ntahondi (wa pili kutoka kushoto)akisoma dua leo kabla ya kuanza kwa Kikao cha Robo ya Kwanza cha Baraza la Madiwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...