Serikali yagharamia kwa asilimia 100

Wafikia asilimia 94

Mradi wa upanuzi wa barabara ya Morogoro sehemu ya Kimara-Kibaha kwa njia nane (Km 19.2), unaendelea vizuri na kwa sasa umefika asilimia 94

Mradi huu unafadhiliwa na Serikali kwa asilimia mia moja na gharama yake ni takriban Shilingi Bilioni 161 ukitarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba nwaka huu.

Aidha, Serikali imeshamlipa Mkandarasi malipo ya zaidi ya Shilingi bilioni 149. 8 ambazo ni sawa na asilimia 93 kulingana na kazi aliyoifanya.

Hadi sasa kazi zilizobakia zikiwa ni kuweka taa za kuongozea magari, Taa za kuangaza barabarani, kuweka kingo (kerbstobne) na kutenga njia zinazoelekea mjini na zinazotoka mjini na kumalizia lami kipande cha kilometa 4 kutoka eneo la Gogoni- Kibamba hadi Kibaha.

Mradi huu unatekelezwa na Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), ambapo lengo lake kubwa ni kupunguza msongamano kwa wasafiri na wasafirishaji wanaongia katikati ya jiji la Dar es Salaam.

kukamilika kwa mradi huu kutaunganisha nchi yetu na nchi jirani za Rwanda, Burundi, Congo na Malawi.

Mradi huu ulianza mwaka 2018 na unajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Estim kutoka Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...