Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Selemani Jafo akihutubia kwenye Mkutano wa Uzinduzi wa ‘Middle East Green Initiatives’ uliofanyika mjini Riyadh nchini Saudi Arabia


Washiriki wakifuatilia Mkutano wa Uzinduzi wa ‘Middle East Green Initiatives’ uliofanyika mjini Riyadh nchini Saudi Arabia


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Selemani Jafo (wa pili kushoto) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Saudia, Mhe. Ali Jabir Mwadini (kushoto) na viongozi wengine walioshiriki Mkutano wa Uzinduzi wa ‘Middle East Green Initiatives’ uliofanyika mjini Riyadh nchini Saudi Arabia jana.

…………………………………………………………….

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Selemani Jafo amesema kuwa Tanzania imejidhatiti katika kujenga uchumi wa kijani na kuzingatia uhifadhi wa mazingira.

Jafo amesema hayo jana katika Mkutano wa Uzinduzi wa ‘Middle East Green Initiatives’ uliofanyika mjini Riyadh nchini Saudi Arabia na kuhudhuriwa na viongozi wa mataifa mbalimbali na mashirika ya kimataifa.

Waziri Jafo alisisitiza kuwa Tanzania imejipanga kutekeleza uchumi wa kijani kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira katika kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo matumizi ya nishati jadidifu kwa lengo la kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kama vile Mradi wa umeme wa Maji wa Mwalimu Nyerere.

Kwa upande wake Mwana Mfalme Mohammed Bin Salman alisema Saudi Arabia na Mataifa ya Mashariki ya Kati yameanzisha Mpango wa ‘Middle East Green Initiative’ kwa lengo la kushirikiana na mataifa mbalimbali katika kukuza uchumi wa kijani na kushirikiana na Jumuiya ya Kimataifa kupambana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la kujenga uchumi endelevu.

Mkutano huo ulioandaliwa na Serikali ya Saudi Arabi, uliongozwa na Mwana Mfalme na Makamu Waziri Mkuu wa Saudi Arabia, Mohammed Bin Salman.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...