Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dk. Abdallah  Salehe Possi amefungua rasmi Onesho la Utalii la My Tanzania Roadshow 2021 lililoanza leo katika mji wa Frankfurt nchini Ujerumani. Onesho hili litafanyika katika nchi tatu zikiwemo  Ujerumani, Austria na Switzerland kwa muda wa siku 6 kuanzia 25-30/10/2021 ambapo Ujumbe wa Tanzania wenye jumla ya Kampuni za Utalii 28 pamoja na taasisi za TANAPA na Ngorongoro utakutana Wafanyabiashara ya Utalii (Travel Agents) wapatao 150. Mhe. Balozi Possi ameahidi kutoa ushirikiano wa kuendelea kutangaza utalii kupitia njia mbali mbali ikiwemo mikutano ya kimtandao pamoja na vyombo vya habari ili kuhakikisha idadi kubwa ya watalii kutoka nchi zinazozungumza lunga ya kijerumani wanatembelea Tanzania.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...