Khadija Kalili, Mafia
Timu ya Nyika FC ya  Kibaha  imeibuka mshindi katika fainali za michuano ya Ligi Mabingwa Mkoa wa Pwani kwa kuichapa Kerege FC bao mbili kwa nunge.

 Kufuatia ushindi huo Nyika FC watacheza na Mabingwa  kutoka katika Mkoa  mingine  kwenye michuano ya RCL .

Nyika FC  ilikutana na vijana wa Kerege wenye maskani yao Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani katika mechi iliyochezwa jana jioni katika Uwanja wa Dawindege Kilindoni Wilayani Mafia Mkoa wa Pwani.
Mchuano  huo  ulikuwa mkali  ambapo pande zote walicheza kwa kukamian kuwania nafasi hiyo ambapo mwanzo wa mchezo hadi mwisho wachezaji wa Kerege FC waliumudu mpira ipasavyo lakini bahati ya kuzitikisa nyavu za  timu ya  Nyika  FC  haikuwa yao hali iliyowafanya vijana wa Kerege  kutoka vichwa chini
hadi kipenga cha mwisho kilipopigwa na aliyekuwa Mwamuzi wa mechi hiyo Ally Mangunga.
Kwa ushindi huo Nyika FC watacheza Ligi Daraja la tatu  huku  michuano hiyo  ikiwa imeandaliwa na Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani  (COREFA)

 Akizungumza na Michuzi Blog  baada ya mechi Kapteni wa timu ya Kerege FC Chande Makoja alisema kuwa  yeye na wenzake walicheza  Ili waweze kupata ubingwa  lakini bahati haikuwa kwao  wanamshukuru Mungu kwa yote.

Wakati huohuo Meneja wa Timu ya Kerege FC Nassir Mohammed amelalamikia  namna mchezo mzima ulivyochezeshwa pamoja na matokeo ya mechi hiyo huku akilalamika ubovu wa kiwanja  ambacho mechi hiyo ilichezwa  huku akilalamika kuwa Kerege FC  waliandaliwa  hujuma ya kukwamishwa lakini  waliingia Uwanjani huku wakiwa tayari wakijua wanakwenda kuang'olewa lakini waliamua kutimiza wajibu wao wa kucheza.
Kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira Mkoa wa Pwani    (COREFA) Ibrahim   Gama aliyekuwepo mwanzo hadi mwisho wa mechi hiyo alisema kuwa amepokea malalamiko kutoka kwa uongozi wa  Kerege FC na kuwataka wafuate taratibu ya kutoa vithibitisho dhidi ya tuhuma hizo na COREFA watachunguza na haki itatendeka .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...