Mwenyekiti wa Tamstoa Chuki Shaban akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya uuzaji magari BE FORWARD wakiwa katika picha ya pamoja jijini Arusha.


Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV- Arusha 

WATUMIAJI wa vyombo vya moto nchini wametakiwa  kutii sheria bila shuruti ili kupunguza ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikipoteza nguvu kazi nyingi.

Hayo yamesemwa na  Mkurugenzi Mtendaji  wa Kampuni ya kimataifa ya uuzaji wa magari  ya BE FORWARD yenye makao yake  makuu jijini Dar es Saalam,Daniel Japhet  wakati akitoa elimu  kwa wananchi waliotembelea Banda lao  katika uwanja wa Stadium jijini Arusha.

Amesema  kuwa,endapo watumiaji wa barabara watatii sheria bila shuruti  itapunguza Sana ajali zinazoweza kuepukika.

“Sisi kama wadau wa kuuza magari Tanzania tunahamasisha watumiaji kutii sheria na kufuatia sheria za usalama barabarani ikiwemo kuzitumia bidhaa zetu kwani zina ubora wa hali ya juu  na huo ndo ukweli na uwazi sisi hatuna biashara ya longolongo tunajiamini kwa kile tunachokifanya,"amesema Daniel.

Amesema wao kama wauzaji wa magari Tanzania wameona watoe sehemu ya faida yao kwa ajili ya kuja kutoa elimu kwa watumiaji wa vyombo vya moto katika kuwahamasisha kufuatia sheria na kanuni ili kuepukika kwa ajali.

“Tumekuwa tukitengeneza wastani wa magari elfu nane hadi elfu kumi  kwa mwezi ambapo tumekuwa tukitumia bandari ya Dar es Saalamu Zambia na Malawi, hivyo tunawaomba Sana  wananchi wajitokeze kwa wingi kutuunga mkono kwa kununua bidhaa zetu kwani ni za uhakika na Zina ubora wa hali ya juu,”amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti  wa wamiliki wa malori wadogo na wa kati,(TAMSTOA)Chuki Shabani  amesema kuwa chama  hicho kipo Kama ngazi kati ya Serikali na wanachama  katika kushirikiana kutoa elimu  kwa wafanyabiashara wasafirishaji wa malori  juu ya umuhimu wao katika kufuata sheria .

Amesema kuwa, madereva malori wamekuwa wakisoma mara kwa mara  kwa ajili ya  kujikumbusha jinsi ya kufuata sheria na kanuni za usalama barabarani na kuepukana na ajali za mara kwa mara.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...