Na WAMJW- Mwanza

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima amefanya ziara ya kukagua Maendeleo ya jengo la mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza- Sekou-Toure.

Katika ziara hiyo ameagiza kasi iendelee katika kukamilisha mradi huo ambao sasa uko asilimia 88 na huduma za uzazi zianze kutolewa katika jengo hilo kabla ya Januari, 2022 kama Mkandarasi alivyoahidi.

Dkt. Gwajima ameelekeza kuanzishwe daftari la kuandika taarifa ya kilichotekelezwa Kila siku ili kuweza kuongeza kasi na kujua kila hatua katika mradi huo ili kuongeza uwajibikaji.

Katika ziara hiyo Dkt. Gwajima aliambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Lutachunzibwa.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...