Na.Khadija Seif, Michuzi TV

BARAZA la Sanaa la Taifa(BASATA) limetoa siku tatu Kwa wadau wa Muziki nchini kutoa maoni yao juu ya vipengele (categories) vya Tuzo za Muziki.

 Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Matiko Mniko wakati wa Mkutano wake na waandishi Wahabari uliofanyika katika makao makuu ya ofisi zilizopo Kivukoni jijini Dar es salaam.

Aidhaa Mniko amevitaja vipengele vitakavyoshindaniwa katika Tuzo hizo na kufafanua kuwa Kuna vipengele 23 na ndani yake Kuna jumla ya Tuzo 52.

Tuzoo hizo zilizinduliwa januari 28 mwaka huu na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo ,Mhe.Mohammed Mchengerwa jijini Dar es salaam zinazotarajiwa kutolewa Marchi 26 mwaka huu baada ya washindi kupatikana kutokana na kura zitakazopigwa na wadau wa Muziki Kwa njia ya Mtandao.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...