Mhe Abubakar Kunenge ameeleza kuwa  Mhe Rais Samia Suluhu Hassan  amedhamiria kuhakisha kuwa anaboresha maisha ya Watanzania na kuondoa kero zao kwa kuleta Ustawi kwenye shughuli za kijamii na Kiuchumi. Ameyasema hayo leo Januari 16, 2022 wakati akikagua Daraja la Mbuchi  lililopo Wilayani Kibiti. 

"Tunajivunia Daraja hili la  Mbuchi linalojengwa kwa Gharama ya Shilingi Bilioni 6.245 litakuwa na urefu wa mita 61,  pamoja na Matengenezo ya Barabara hii ya Muhoro -Mbuchi- Mbwera ya urefu wa kilometa 23 kwa sasa Ujenzi umefikia asilimia 80". 

"Mhe Rais ameamua kuifungua Pwani kufika kusiko fikika" ameongeza kunenge.  

Kunenge ametaja kuwa uwepo wa Daraja hilo kutachochea shughuli za kiuchumi ikiwemo  utalii,Uvuvi na kilimo Biashara. 

ametoa rai kwa mkandarasi kufanya kazi usiku na Mchana na kukamilisha Ujenzi kwa wakati ifikapo Februari 23, 2022

Kunenge amewataka wananchi  kutojihusisha na Wizi wa vyuma vya Daraja hilo.














Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...