Kaimu Meneja Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mara Bw. Robert Busumabu akichangia hoja wakati wa semina kuhusu taratibu za forodha zinazotumika kuwahudumia wafanyabiashara wa kati na wadogo wanaotumia Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Semina hiyo imefanyika kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.
Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Edwin Iwato akitoa elimu ya taratibu za forodha zinazotumika kuwahudumia wafanyabiashara wa kati na wadogo wanaotumia Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Elimu hiyo imetolewa kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.
Afisa Msimamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Lameck Ndinda akitoa mafunzo ya huduma bora kwa wateja kwa watumishi wanaofanya kazi katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Mafunzo hayo yametolewa kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.
Afisa Uhusiano kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi Salome Mwandalanga akimsikiliza kwa makini mfanyabiashara wa Sirari Bw. Joseph Mokare wakati wa kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea katika Wilaya ya Tarime mkoani Mara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...