Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu Tanzania(NBAA) imeendelea kutoa elimu/mafunzo kwa wanafunzi wa Taasisi, Vyuo pamoja na Shule za Sekondari ikiwa na lengo la kuwajengea ufahamu kuhusu shughuli mbalimbali za Bodi na kukuza taaluma ya uhasibu.

Akizungumza na Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Kodi (ITA) wakati wa kutoa mafunzo hayo Afisa wa NBAA kutoka Idara ya Elimu na Mafunzo, Ibrahim Magambo amesisitiza kuwa si kila aliyesomea uhasibu anaweza kufanya kazi za kihasibu bali inabidi kufanya mitihani ya Bodi hiyo ili kupewa cheti cha kitaaluma ili uweze kutambulika kama Mhasibu na kuweza kufanya kazi nje na ndani ya nchi, wanafunzi wa Kozi nyingine ambazo hazihusiani na masomo ya Uhasibu nao wana nafasi ya kufanya mitihani ya Bodi na wataanzia masomo ya ngazi ya kwanza (foundation level) tofauti na wale waliosomea masomo ya Uhasibu  na pia waliomaliza kidato cha nne na sita na wanacheti wanaweza kufanya mitihani ya Bodi

Afisa wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu Tanzania(NBAA) kutoka Idara ya Elimu na Mafunzo, Ibrahim Magambo akitoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Kodi (ITA) jijini  Dar es Salaam ikiwa ni lengo la kutoa elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo kwa Taasisi, Vyuo pamoja na Shule za Sekondari.
Afisa Masoko na Mawasiliano wa NBAA Magreth Kageya akitoa ufafanuzi kuhusu kazi zinazofanywa na bodi hiyo wakati wa mafunzo kwa Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Kodi (ITA) Jijini Dar
Baadhi ya Waalimu wa Chuo hicho pia walipata fursa yakuelezea ni namna gani pia wao waliweza kupata CPA na kutoa elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo pamoja na namna ya kuweza kupata CPA.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Kodi (ITA) wakifuatilia mada kutoka ka maofisa wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi Hesabu Tanzania(NBAA) waliofika chuoni hapo kwa ajili ya kutoa elimu kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi hiyo pamoja na namna ya kuweza kupata CPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...