Na Amiri Kilagalila,Njombe

Timu ya Chama la wana ya mjini Makambako mkoani Njombe imetwaa kombe la B2K cup katika michuano hiyo iliyodhaminiwa na kampuni ya shikamoo Parachichi na kukabidhiwa zawadi ya Ng'ombe baada ya kuifunga timu ya jeshi la polisi Makambako kwa mikwaju ya penati 4 kwa 3.

Akizungumza wakati akikabidhi zawadi mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa wilaya ya Njombe Bi Kissa Kasongwa amemshukuru mkurugenzi wa shikamoo parachichi Erasto Ngole kwa kudhamini ligi hiyo na kuhakikisha vijana wanakusanyika pamoja na kudumisha amani na upendo kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Mkuu wa wilaya hiyo amekabidhi Ng'ombe kwa mshindi wa kwanza wa ligi hiyo ambayo ni timu ya chama la wana,huku mshindi wa pili timu na polisi Makambako ikikabidhiwa mbuzi wa wiwili na Mshindi wa tatu Goldeni ballers imekabidhiwa mpira huku marefa,mfungaji bora,mchezaji mwenye nidhamu wote kwa pamoja wamekabidhi zawadi pia.

Balozi wa kampuni ya shimoo Parachichi ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za kizazi kipya Batwery kinyunyu (B2K) amemshukuru mkuregenzi huyo Ngole kwa kudhamini ligi hiyo na kueleza kuwa lengo kubwa la ligi hiyo ilikua ni kuhamasisha vijana kujiajiri katika kilimo cha parachichi ambacho kimekua na tija kubwa mkoani njombe .

Licha ya kudhamini ligi hiyo mkurugenzi wa kampuni ya shikamoo Parachichi Elasto Ngole ambaye ni katibu wa siasa na uenezi (CCM) mkoa wa Njombe ameahidi kutoa zaidi ya milioni tatu ili kuhakikisha msanii huyo B2K ananunua camera ambazo zitamuwezesha kufungua studio ya kurekodia video ili aweze kuwasaidi vijana wote ambao wanajihusisha na tasnia hiyo ya uimbaji wa nyimbo za kizazi kipya na zile za injili.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...