Na. John Mapepele

Naibu Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Saidi Yakubu ameutaka uongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kuifanya taasisi hiyo kuwa kituo chenye hadhi ya kimataifa kwenye utoaji wa taaluma  ya Sanaa na utamaduni kuliko ilivyo sasa

Yakubu amesema hayo leo Februari 7, 2022 alipofanya ziara chuoni hapo na kuongea na watumishi  na Menejimenti ya TaSUBa na baadaye kukagua shughuli mbalimbali  zinazotekelezwa na taasisi hiyo.

Amefafanua kuwa kutokana na upekee wa taaluma zinazotolewa na chuo hicho ambazo zinaendana  na vyuo vya kimataifa hakuna sababu ya chuo hicho kubaki na hadhi yake ya sasa inayoongozwa na dira ya kutoa taaluma katika ubora kwa ngazi ya Afrika.

" Ni wazi kwamba  kwa upekee wa chuo chetu na kozi zinazotolewa hapa ni lazima tuondokane na  na fikra za Bagamoyo, Tanzania au hadhi ya Afrika na badala yake tuwe wa kimataifa " ameongeza Yakubu.

Ameutaka uongozi kuwa mbunifu kwa kutumia raslimali za wizara mama kujitanua  zaidi nchi nzima badala ya kufikiria  eneo la Bagamoyo pekee.

Amekitaka chuo kuongeza udahili wa wanachuo ili hadhi ya chuo hicho iwe ya kimataifa ambapo amesisitiza  kuwachukua pia wanafunzi kutoka nje ya Tanzania ili wawe mabalozi wa kukitangaza chuo katika nchi zao.





 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...