Huku
zikiwa zimebaki takriban wiki tatu tu kabla ya kufanyikka kwa mbio za
20 za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2022, waandaaji wa mbio hizo
wamewakumbusha washiriki kuwa usajili unafungwa Jumatatu Februari 7,
2022.
Taarifa
iliyotolewa jana Jijini Dar es Salaam, ilisema usajili utafungwa rasmi
Februari 7, 2022 saa sita ya usiku na kuwataka ambao hawajajisajili
kutumia muda uliobaki kujisajili kwa njia ya mtandao ili kuepukana na
usumbufu.
“Usajili
ni kwa njia ya mtandao kwa kupitia tovuti yetu ya
www.kilimanjaromarathon.com au Tigo Pesa kwa kupiga *149*20#. Mtandao
hautafanya kazi baada ya Februari 7, 2022 kwa hivyo ni bora watu watumie
muda uliobaki kufanya usajili,” walisema waandaaji hao.
Hata
hivyo walisema usajili wa mbio za Grand Malt za Km 5 maarufu kama Fun
Run utaendelea hata baada ya tarehe hiyo iliyotajwa na pia katika vituo
vya kuchukulia namba za kukimbilia.
“Tunapenda
pia kuwakumbusha washiriki kuwa endapo nafasi zitajaa kabla ya Februari
7, 2022 basi tutalazimika kufunga usajili mara moja, ilisema taarifa
hiyo ya waandaaji.
Walisema
watatangaza tarehe na vituo ambapo washiriki watachukua namba za
kukimbilia kwa mikoa ya Dar es Salaam,Arusha na Kilimanjaro. The
organizers said that soon they will announce race number collection
points and dates in Dar es Salaam, Arusha and Moshi.
Wadhamini wa mbio za Kilimanjaro Marathon 2022 ni Kilimanjaro Premium Lager (Mdhamini Mkuu) Tigo (21km) na Grand Malt (5km).
Wadhamini
wa meza za maji ni pamoja na Absa Tanzania, Unilever Tanzania, TPC
Sugar, Simba Cement na Kilimanjaro Water. Wasambazaji rasmi ni
GardaWorld Security, Keys Hotel, Kibo Palace Hotel, CMC Automobiles na
Surveyed Plots Company Ltd (SPC) na Bodi ya Utalii (TTB).
Katika
hatua nyingine, Kwa mujibu wa waandaaji wa Kilimanjaro Marathon, kwa
mara ya kwanza kutakuweko na maonesho yanayojulikana kama Kili Expo (The
People's Expo) ambapo wadhamini na wadau wengine wa mbio hizo watapata
fursa ya siku tatu za kuonyesha bidhaa na huduma wanazotoa, maonyesho
ambayo yanatarajiwa kufanyika kati ya Februari 24-26, 2022, katika
viwanja vya MoCU.
"Maonyesho
haya pia linakusudiwa kuwapa umma uzoefu wa muda mrefu wa mbio za Kili
Marathon; pia kwa mwaka huu wanaotarajia kushiriki mbio hizo watapata
fursa ya kuchukua namba zao za ushiriki eneo la chuo kikuu cha Ushirika
badala ya eneo la hotel kama ilivyokuwa miaka ya nyuma”, ilisema taarifa
hiyo ya wandaaji.
Mbio
za Kilimanjaro Premium Lager Marathon, zinatarajiwa kufanyika Jumapili
ya Februari 27, 2022, katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi
(MoCU), ambapo zimeandaliwa na taasisi ya Kilimanjaro Company Limited na
kuratibiwa na wadau wa hapa nchini kampuni ya Executive Solutions
Limited.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...