Na. John Mapepele


Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Dkt, Hassan Abbasi amepamba hafla ya  Usiku wa Mahaba  ndi ndi ndi  baada ya kuandaliwa keki maalum ya siku yake ya kuzaliwa na kuimbiwa wimbo wa kuzaliwa ulioongozwa na Diamond Platnumz.

Dkt. Abbasi alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa waliokuja kushiriki kwenye hafla hiyo tarehe 14 Februari 2022 ambayo ni siku ya wapendanao (Valentine) na ghafla mshereheshaji wa hafla hiyo  Zembwela kutangaza kuwa wasafi wameandaa keki maalum kwa Dkt Abbasi.
 
Kwa upande wake Dkt. Abbasi aliishukuru Wasafi kwa kitendo hicho cha kumpa keki na kumwimbia wimbo wa kuzaliwa.

" Ndugu zangu niseme  wazi kuwa sikutegemea wala kuwaza hii surprise, ninawashukuru sana, kitendo mlichonifanyia hakiwezi kunitoka kwenye kumbukumbu za maisha yangu." Alisisitiza Dkt. Abbasi.

Katika hafla hiyo wasanii mbalimbali walitumbuiza  huku msanii maalum wa siku Zuchu  akikonga  nyoyo za washabiki  huku mamake bi Hadija Kopa na Bosi wake Diamond Platinum wakiimba pamoja kwenye baadhi ya nyimbo na kushangiliwa na umati wa washabiki.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wanasiasa na watu mashuhuri.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...