Mwamvua Mwinyi,Pwani
WATU
 wawili wamefariki dunia pamoja na kujeruhi wengine wawili ,katika ajali
 iliyohusisha magari matatu kugongana huko maeneo ya Miwaleni, 
Halmashauri ya wilaya Kibaha Vijijini mkoani Pwani.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa polisi Mkoani Pwani,Pius Lutumo alieleza, ajali hiyo imetokea march 28 asubuhi.
Alieleza
 kuwa, gari namba T608 AGV  likiwa na tela lenye namba T.317 AQM aina ya
 scania likiendeshwa na Raymond Kimaro (36) ,mkazi wa Ubungo likitokea 
nchini Kongo kwenda Dar es salaam ambapo lilihamia upande wake wa 
barabara na kugonga gari namba T.256 CMF aina ya Noah iliyokuwa ikitokea
 Dar es Salaam kwenda Morogoro.
Alieleza,hali
 hiyo ilisababisha kontena kuchomoka na kuangukia gari SU 38223 aina ya 
Toyota land cruiser iliyokuwa ikitokea Dar es salaam kwenda Morogoro 
ikiendeshwa na Innocent Gerson Mringo na kusababisha vifo na majeruhi 
hao.
Lutumo alitaja 
waliofariki dunia kuwa ni profesa Prosper Ngowi (55) mhadhiri wa Chuo 
Kikuu cha Mzumbe, Na Innocent Gerson (33) mkazi wa Dar es Salaam na 
dereva.
Majeruhi ni 
Raymond Kimaro (39) dereva wa lori T.608 AGV na Abdallah Mohammed 
(33)dereva wa Noah mkazi wa Dar es Salaam na kusababisha uharibifu wa 
magari.
Kamanda huyo 
alifafanua, chanzo Cha ajali bado kinachunguzwa hata hivyo uchunguzi wa 
awali unaonyesha Kuwa ni uzembe wa dereva wa gari aina ya scania kuhama 
upande wake wa barabara na kugonga gari aina ya Noah na kupelekea 
kontena kuchomoka na kuliangukia gari Toyota cruiser.
Lutumo
 alisema, mwili wa marehemu profesa Prosper Ngowi umehifadhiwa hospital 
ya rufaa Tumbi na mwili wa marehemu Innocent Gerson umehifadhiwa katika 
kituo cha afya Mlandizi.
Majeruhi wametibiwa na hali zao ni nzuri huku mtuhumiwa akishikiliwa na jeshi la polisi kwa hatua zaidi.
Lutumo aliwaasa madereva kuacha kuendesha pasipo kufuata Sheria za Usalama Barabarani,na wawe makini ili kujiepusha na ajali.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...