Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
MKOA
wa Pwani umeanza operesheni ya kukamata wahamiaji haramu kwenye mkoa
huo,ili kupunguza ama kuondoa wimbi la wahamiaji hao wanaoingia kupitia
njia za panya pasipo kufuata sheria.
Operesheni hiyo ,Ni utekelezaji wa agizo la Inspekta Jenerali wa Uhamiaji Nchini Anna Makakala , alilolitoa ili kusaidia kuchunguza na kubaini wahamiaji haramu na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria ,kuchukuliwa hatua stahiki.
Akizungumza
na maofisa Uhamiaji wa mkoa huo, mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari
Kunenge alisema zoezi hilo litakuwa zoezi maalumu ambalo litaisha Machi
23 mwaka huu.
Vilevile, alieleza zoezi hilo litagusa kwenye maeneo ya uwekezaji hivyo wawekezaji wanapaswa kutoa ushirikiano ili kufanikisha.
"Kwa
kuwa taratibu za kuishi nchini zipo ni vema wageni wakazifuata kwani
hakuna sababu ya wageni kuingia au kuishi kinyume cha
sheria,"alifafanua.
Naye
ofisa Uhamiaji wa mkoa wa Pwani Omary Hassan alisema kuwa baadhi ya
wahamiaji haramu hutafuta fursa za ajira hasa wanaotoka pembe ya Afrika
ikiwemo Ethiopia huwa wanapita kwenda Kusini mwa Afrika kutafuta maisha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...