Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha March 23
WAKAZI
wa kata ya Pangani , Kibaha Mjini Mkoani Pwani pamoja na Diwani wa kata
hiyo Agustino Mdachi wameeleza Hali mbaya ya upatikanaji huduma ya maji
safi na salama ,kwakuwa wanataabika kutumia maji ya visimani,mtoni
,kwenye madimbwi ama kununua dumu na ndoo kwa sh.500.
Hali
hiyo imewapa taabu kwa kipindi kirefu kwani licha ya Kuwa katika Mji wa
Mjini yaani Kibaha Lakini ni kata iliyokuwa inakosa huduma ya maji.
Hayo
yalibainika ,wakati baadhi ya wajumbe kamati ya siasa CCM mkoa na
kamati ya siasa mji wa Kibaha ,iliposhiriki ukagua ujenzi wa mradi wa
kituo cha afya Kidimu na mradi wa tenki la maji Vikawe, kata ya Pangani
utakaojumuisha ujenzi wa matenki makubwa ya ujazo wa lita milioni tano
pamoja na usambazaji kwa watumiaji tenki la Vikawe ikiwa ni sehemu ya
mradi huo wa matenki matatu.
Diwani
wa kata ya Pangani, Mdachi alisema ,kwasasa Wana matumaini ya
kuondokana na kero hiyo baada ya mradi wa tenki la maji Vikawe,
kukamilika kwa asilimia zaidi ya 90.
"Hali
Ni mbaya ,kwani Halmashauri ya Mji wa Kibaha changamoto kubwa ya maji
ipo kata ya Pangani ,Ila Hali ya mradi inatumainisha upo kwenye asilimia
zaidi ya 90 na tumeelezwa ifikapo mwezi wa sita mwaka huu kero hii
itabaki historia."
"Serikali
imetambua uhitaji wetu ,Tunashukuru Sana ,nimekuwa nisali usiku na
mchana moja ya changamoto za kata hii ziishe ili nami Kama diwani niweze
kusema Jambo katika utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM"
Akizungumzia
ujenzi wa kituo cha afya Kidimu ,Mdachi alisema kata hiyo ilikuwa haina
kituo cha afya, wakazi wa kata hiyo wanafuata huduma za afya umbali
mrefu kituo cha afya Mkoani na hospital ya rufaa ya mkoa Tumbi.
Alisema, ujenzi ulipofikia asilimia 50 pia wanatarajia kuondokana na adha ya kufuata huduma za kiafya umbali mrefu.
Mkazi wa Kidimu ,kata ya Pangani ,Bahati Omar alieleza wana matumaini kwa Sasa baada ya kuona ujenzi unakamilika wa maji .
"Tulikuwa
tunatoka majumbani unakwenda kuchimba vijisima ili kupata maji ,uwezo
wetu wengine sisi Ni wa Hali ya chini hatumudu sh .500 kwa ndoo ,unajua
matumizi ya nyumbani ndoo kwa siku ziwe japo tano hapo kupikia, matumizi
ya chakula ,usafi ,watoto ,baba yaani hayatoshi ,na huwezi kununua maji
bila chakula ,kiukweli Ni Hali mbaya "
Bahati
alisema kwamba, Rais Samia Suluhu Hassan ametoa milioni 250 kukamilika
ujenzi wa kituo hiki Cha afya Kidimu kupitia fedha za tozo ,wanashukuru
kwakuwa Ni mkombozi kwa afya za watoto na wanawake ambao kwa kiasi
kikubwa wanapata shida.
Mhandisi
kutoka DAWASA Kibaha,Fred Mushi alieleza ,awamu ya kwanza mradi
utalisha mitaa vya Vikawe Shule, Vikawe Bondeni Kidimu Miwalebaada ya
hapo wakikabidhi dawasa itafikisha mitaa mingine ikiwemo mtaa wa
Mkombozi.
"Hatua iliyopo Ni usukumaji maji na tunatarajia ujenzi kukamilika June 2022"alifafanua Mhandisi Fred.
Mwenyekiti wa CCM Pwani ,Ramadhani Maneno CCM imetoa maelekezo mikoa ipitie miradi kisha ipeleke taarifa kwa mkuu wa mkoa.
"Mimi
na wenzangu mkoa tumejigawa ,tumepitia miradi ,tumeridhishwa na
utekelezaji Lakini nasisitiza miradi iendane na thamani ya fedha
"Mh.Rais ametoa fedha hizi zitumike kwa malengwa sahihi "alieleza
Maneno.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini, Maulid Bundala alielekeza mradi wa
ujenzi wa kituo cha afya ikamilike mwezi ujao ili itoe huduma haraka na
mhandisi wa DAWASA wakamilishe mradi Kama walivyoahidi June 16 mwaka
huu.
Mkurugenzi wa
Halmashauri mji Kibaha, Mshamu Munde alisema wanasimamia miradi
kikamilifu na wataalamu wa Halmashauri wanaendelea kufanya majukumu yao
ili kuhakikisha inaleta tija kwa wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...