Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha March 23

WAKAZI wa kata ya Pangani , Kibaha Mjini Mkoani Pwani pamoja na Diwani wa kata hiyo Agustino Mdachi wameeleza Hali mbaya ya upatikanaji huduma ya maji safi na salama ,kwakuwa wanataabika kutumia maji ya visimani,mtoni ,kwenye madimbwi ama kununua dumu na ndoo kwa sh.500.

Hali hiyo imewapa taabu kwa kipindi kirefu kwani licha ya Kuwa katika Mji wa Mjini yaani Kibaha Lakini ni kata iliyokuwa inakosa huduma ya maji.


Hayo yalibainika ,wakati baadhi ya wajumbe kamati ya siasa CCM mkoa na kamati ya siasa mji wa Kibaha ,iliposhiriki ukagua ujenzi wa mradi wa kituo cha afya Kidimu na mradi wa tenki la maji Vikawe, kata ya Pangani utakaojumuisha ujenzi wa matenki makubwa ya ujazo wa lita milioni tano pamoja na usambazaji kwa watumiaji tenki la Vikawe ikiwa ni sehemu ya mradi huo wa matenki matatu.

Diwani wa kata ya Pangani, Mdachi alisema ,kwasasa Wana matumaini ya kuondokana na kero hiyo baada ya mradi wa tenki la maji Vikawe, kukamilika kwa asilimia zaidi ya 90.

"Hali Ni mbaya ,kwani Halmashauri ya Mji wa Kibaha changamoto kubwa ya maji ipo kata ya Pangani ,Ila Hali ya mradi inatumainisha upo kwenye asilimia zaidi ya 90 na tumeelezwa ifikapo mwezi wa sita mwaka huu kero hii itabaki historia."

"Serikali imetambua uhitaji wetu ,Tunashukuru Sana ,nimekuwa nisali usiku na mchana moja ya changamoto za kata hii ziishe ili nami Kama diwani niweze kusema Jambo katika utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM"

Akizungumzia ujenzi wa kituo cha afya Kidimu ,Mdachi alisema kata hiyo ilikuwa haina kituo cha afya, wakazi wa kata hiyo wanafuata huduma za afya umbali mrefu kituo cha afya Mkoani na hospital ya rufaa ya mkoa Tumbi.

Alisema, ujenzi ulipofikia asilimia 50 pia wanatarajia kuondokana na adha ya kufuata huduma za kiafya umbali mrefu.

Mkazi wa Kidimu ,kata ya Pangani ,Bahati Omar alieleza wana matumaini kwa Sasa baada ya kuona ujenzi unakamilika wa maji .

"Tulikuwa tunatoka majumbani unakwenda kuchimba vijisima ili kupata maji ,uwezo wetu wengine sisi Ni wa Hali ya chini hatumudu sh .500 kwa ndoo ,unajua matumizi ya nyumbani ndoo kwa siku ziwe japo tano hapo kupikia, matumizi ya chakula ,usafi ,watoto ,baba yaani hayatoshi ,na huwezi kununua maji bila chakula ,kiukweli Ni Hali mbaya "

Bahati alisema kwamba, Rais Samia Suluhu Hassan ametoa milioni 250 kukamilika ujenzi wa kituo hiki Cha afya Kidimu kupitia fedha za tozo ,wanashukuru kwakuwa Ni mkombozi kwa afya za watoto na wanawake ambao kwa kiasi kikubwa wanapata shida.
 
Mhandisi kutoka DAWASA Kibaha,Fred Mushi alieleza ,awamu ya kwanza mradi utalisha mitaa vya Vikawe Shule, Vikawe Bondeni Kidimu Miwalebaada ya hapo wakikabidhi dawasa itafikisha mitaa mingine ikiwemo mtaa wa Mkombozi.

"Hatua iliyopo Ni usukumaji maji na tunatarajia ujenzi kukamilika June 2022"alifafanua Mhandisi Fred.

Mwenyekiti wa CCM Pwani ,Ramadhani Maneno CCM imetoa maelekezo mikoa ipitie miradi kisha ipeleke taarifa kwa mkuu wa mkoa.

"Mimi na wenzangu mkoa tumejigawa ,tumepitia miradi ,tumeridhishwa na utekelezaji Lakini nasisitiza miradi iendane na thamani ya fedha "Mh.Rais ametoa fedha hizi zitumike kwa malengwa sahihi "alieleza Maneno.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini, Maulid Bundala alielekeza mradi wa ujenzi wa kituo cha afya ikamilike mwezi ujao ili itoe huduma haraka na mhandisi wa DAWASA wakamilishe mradi Kama walivyoahidi June 16 mwaka huu.

Mkurugenzi wa Halmashauri mji Kibaha, Mshamu Munde alisema wanasimamia miradi kikamilifu na wataalamu wa Halmashauri wanaendelea kufanya majukumu yao ili kuhakikisha inaleta tija kwa wananchi.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...