Wafanyabiashara wa Vinywaji 
pamoja na watumiaji wametakiwa kuwa na utaratibu wa kuhakiki Vinywaji 
kwa kutumia app maalumu ya Hakiki stempu ili kutambuwa bidhaa feki 
sokoni ambayo zinaweza kuleta athari kwa mlaji.
Akizungumza mjini
 Babati Mkoani Manyara Balozi wa Kodi Edward Kumwembe amesema 
application ya Hakiki stempu inauwezo wa kutambua uhalali wa bidhaa za 
Vinywaji ambazo zipo sokoni ambapo mtumiaji atapaswa kuwa na Application
 hiyo katika simu janja na kufanya uhakiki kwa kutumia simu yake kama 
iwapo bidhaa hiyo inafaa kwa matumizi ya binadamu.
Kumwembe 
amesema "kuna app maalumu ambayo inapatikana katika hizi simu za 
smartphone ambazo Zina application au maarufu watu wanaita App ambayo 
inahakiki ubora wa Vinywaji vyako, ambayo inahakiki kwa njia mbili wewe 
ukiwa ni mnunuaji kutoka sehemu nyingine unaweza inahakiki Vinywaji 
vyako lakini vilevilie wewe unapomuuzia mtu mwingine mteja naye anaweza 
kuhakiki kwasababu wakati mwingine unaweza kununua kitu ambacho hakina 
ubora lakini siyo kosa lako" 
Aidha Kumwembe amesema lengo la 
kuhakiki ubora wa bidhaa za Vinywaji ni kwa sababu kuna aina nyingi za 
Vinywaji hivyo siyo rahisi kufahamu ubora wa Vinywaji hivyo.
Amesema
 kwa kutumia mfumo huo wa app utaweza kupata taarifa sahihi kuhusu 
ilipotoka bidhaa,ilipotengenezwa,na lini itaisha muda wake wa matumizi 
hivyo kumfanya mlaji wa bidhaa husika kuwa salama.
Kwa Upande 
wake muuzaji wa Vinywaji mbalimbali kutoka Mjini Babati Bw.Naingwa 
ameishukuru mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kutoa elimu juu ya matumizi 
sahihi ya kutumia application hiyo inayoweza kuhakiki ubora na uhalali 
wa Vinywaji na kwamba itawasaidia kuepuka kununua bidhaa feki.
"Application
 hii inafaida nyingi kwa sisi wafanyabiashara hasa pale tunapo kwenda 
kununua Vinywaji kwani itatusaidia kutambuwa Vinywaji feki pamoja na 
kufahamu ubora wa Vinywaji hivyo ili kumlinda mteja"alisema
Hata 
hivyo maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoka Makao Makuu 
wapo Mkoani Manyara kwa siku kumi katika kampeni ya walioiita Mlango kwa
 mlango (Door to door) inayolenga kutoa elimu kwa Wananchi na 
wafanyabiashara juu ya matumizi sahihi ya EFD machine,matumizi ya Hakiki
 stempu inayolenga kutambuwa Vinywaji feki sokoni na msisitizo wa kutoa 
na kudai risiti baada ya kuuza au kununua bidhaa.Balozi wa kodi Bw. Edward kumwembe akifanya zoezi la Hakiki stamp
Balozi wa Kodi Edward kumwembe
Afisa wa TRA akitoa Elimu ya kodi 
Home
HABARI
WAFANYABIASHARA WA VINYWAJI NA WATUMIAJI WATAKIWA KUHAKIKI VINYWAJI KUTUMIA MFUMO MAALUM  'APP'  YA HAKIKI STEMPU KUTAMBUA BIDHAA FEKI SOKONI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...