Kama ilivyokuwa katika miradi mbalimbali ya kimkakati, Benki ya NMB imeendelea kuwa mstari wa mbele kwenye kutoa ushirikiano kwa Serikali na Wakandarasi ili kuhakikisha miradi inayojengwa kwa manufaa ya Watanzania inakamilika kwa wakati.
Katika mradi wa reli ya kisasa ya SGR, Benki ya NMB imeshiriki katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika awamu ya tatu ya ujenzi wa reli hiyo yenye urefu wa kilomita 368 kutoka Makutupora mpaka Tabora. Mbali na kuwa wabia katika mradi huu mkubwa, benki hiyo imedhamini shughuli hii ya uwekaji wa jiwe la msingi iliofanyika katika viwanja vya Cheyo B, Tabora.
Afisa Mkuu wa Rasilimali Watu wa Benki ya NMB – Emmanuel Akonaay akimuelezea Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa, jinsi benki ya NMB ilivyoshiriki katika mradi wa SGR kupitia wakandarasi wa mradi huo kwanzia Dar- Morogoro, Morogora- Dodoma mpaka sasa, Makutupora- Tabora. Pia, namna benki ilivyowawezesha wazabuni wa mradi huo kwa kuwapa mitaji na kuhakikisha watumishi wanalipwa kupitia Benki ya NMB.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...