Kada wa chama cha mapinduzi na mfanyabiashara wa jijini Arusha Nathan Kimaro ametembelewa na Muanzilishi/ Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Media Group Joseph Kusaga kujadili na kubadilishana mawazo ya mambo mbalimbali ya kuwasaidia na kuwajengea uwezo Vijana wa kupata fursa ili waendelee kujiajiri katika nyanja mabalimbali na hatimaye kufikia mafanikio makubwa katika maisha na kusadia kujenga nchi kwa namna moja ama nyingine.
Mbali ya kukutana na Mdau huyo mkubwa wa maendeleo hapa nchini pia Nathan Kimaro alipata fursa ya kukutana na viongozi wa mkoa wa jiji hilo ambao wamekuwa mstari wa mbele kuwasaidia vijana kupata fursa mbalimbali za kujiajiri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...