**********************

Na. John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya wawekezaji wa kujenga miundombinu ya michezo ambao wameonyesha nia ya kujenga miundombinu ya kisasa ya michezo hapa nchini.

Mhe. Mchengerwa ameambatana na Watendaji kadhaa wa Wizara yake kwenye Sekta ya Michezo wakiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini, Yusufu Omary Singo wamekutana na wawekezaji hao na kufanya mazungumzo leo Aprili 22, 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.

Mhe, Mchengerwa amekutana na wawekezaji hao kufuatia dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuinua kiwango cha michezo nchini kufikia ngazi ya kimataifa kwakuwa na mkakati wa kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya michezo kote nchini.

Kwa sasa Serikali inakusudia kujenga miundombi ya kisasa ikiwa ni pamoja na viwanja vya michezo, Sanaa na arena pia kuwa na miundombinu ya kisasa ya michezo kwa shule mbili kila mkoa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...