Na Amiri Kilagalila,Njombe

Mpiga debe mmoja wa eneo la Makambako mkoani Njombe amefariki dunia kwa kukanyagwa na gari katika kichwa chake kutokana na kuanguka wakati akifukuzia basi linalofanya safari zake kutoka Mbeya kwenda mkoani Mwanza ili aweze kupata posho yake ya kupakia abiria.

Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issah amethibitisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

“Mpiga debe alikuwa amefuata fedha yake kwa ajili ya abiria aliokuwa amewapakia na kwa bahati mbaya ule malango wakati unajifunga aliweza kusukumwa na akadondokea kwenye uvungu na tairi za nyuma za gari ziliweza kumpitia”alisema Kamanda Issah

Ametoa wito kwa wafanyakazi wa maeneo ya stendi kuwa makini na kuangalia usalama wao wakati wa kufanya kazi zao.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...