Na John Walter-Manyara 

Mbunge wa Vijana Taifa kutoka mkoa wa Manyara Asia Halamga ametoa msaada wa Karatasi (REEM PAPERS) kwa ajili ya uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi kwenye majimbo yote Matano ya mkoa wa Manyara.

Halamga amekabidhi Karatasi hizo leo Mbele ya Katibu wa NEC, Siasa, Itikadi na uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka Katika ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi mjini Babati.

Amesema Karatasi hizo zitasaidia katika zoezi la kutoa fomu za kugombea nafasi mbalimbali na kuondoa usumbufu wa kusuasua kwa utoaji wa fomu hizo katika majimbo ya mkoa wa Manyara.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Babati Daniel Muhina amemshukuru Mbunge huyo kwa msaada huo akieleza kuwa ametoa katika muda muafaka ambao Chama kinaendelea na chaguzi zake ndani ya Chama.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...