Na Amiri Kilagalila,Njombe

Serikali ya mkoa wa Njombe imezindua zoezi la utoaji wa chanjo ya ugonjwa  wa polio awamu ya pili kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano zoezi ambalo litafanyika kwa siku nne.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Waziri Kindamba ameongoza zoezi hilo kwa kutoa chanjo kwa watoto kwa ushirikiano na wataalamu wa afya katika kituo cha afya cha Njombe mjini na kubainisha kuwa katika awamu ya pili tena watoto zaidi ya laki moja na kumi wanatarajia kupata chanjo hiyo.

“Ni muhimu kulinda na kukinga watoto wetu kwa kuwa hii ndio Tanzania ijayo,tunatakiwa kuwalinda watoto wetu”alisema Kindamba

Vile vile Waziri Kindamba amewapongeza na kutoa zawadi kwa wanaume waliojitokeza kufikisha watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupata chanjo ya ugonjwa wa Polio kwa njia ya matone.

“Wababa kama hawa wamebaki wachache sana,baba ambaye anamsindikiza mama ili mtoto apate chanjo,sina shaka baba wa namna hii hata mama alipokuwa mjamzito alikuwa anaambatana naye kwenda Kliniki”alisema Kindamba

Kindamba amesema katika awamu ya kwanza mkoa wa Njombe umevuka lengo kwa kuchanja watoto kwa 116% huku akibainisha kuwa zoezi hilo linaendelea kwa mikoa minne ya Njombe,Mbeya,Ruvuma na Songwe ambayo ipo jirani zaidi na nchi ya Malawi ulikoanza kuibuka ugonjwa huo.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...