Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, amewataka viongozi mbalimbali wanaofanya ziara hususan katika miradi ya maendeleo kuwapa fursa wananchi kuona kinachofanywa na serikali.

Shaka ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipotembelea soko Kuu la Kariakoo akiwa katika ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, likiwemo Soko la Kariakoo alikoshuhudia hatua nzuri za ukarabatibwake.

"Ndugu zangu viongozi nadhani sasa ni muda mwafaka kubadilika katika hizi ziara, badala ya kukaa na kujifungia na kuzungumza sisi wenyewe, ni vyema tukawapa nafasi wananchi kuona Yale yanayofanywa na serikali yao chini ya Rais Samia Suluhu Hassan," amesema.

Shaka ameipongeza serikali kwa kazi nzuri inayofanya katika ujenzi nabukarabati wa soko hilo ambapo amesema litakapokamilika manufaa yake hayatakuwa kwa Kariakoo pekee bali ni kwa Dar es Salaam na Afrika Mashariki yote.

Awali akimkaribisha Shaka, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ludigija Ng'wilabuzu, aliwapongeza wakandarasi wa mradi huo kwa kuutekeleza kwa kasi.

Amesema mradi huo upo chini ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambapo amesema kazi inaendelea vizuri na anaamini itakamilishwa katika muda muda wa makubaliano.











 







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...