Raisa Said , Korogwe


Wananchi wa wilaya ya Korogwe wametahadharishwa juu ya athari za kutozingatia maelekezo ya wataalamu wa Afya yanayohusiana na Elimu ya Afya ya Uzazi hususani ujauzito na kujifungua kwa wanawake wanaobeba Ujauzito wa Kwanza na wale wanaobeba ujauzito katika Umri mdogo

Tahadhari hiyo imetolewa na Mbunge wa Korogwe Vijijini Timotheo Mzava
mara baada ya kufika Kijiji Cha Kizara na kufuatilia msichana mmoja
mwenye umri wa miaka 15 kupoteza mtoto baada ya kucheleweshwa
kupelekwa kwenda kituo cha afya kilichopo Magoma. .


Mbunge huyo alisema kuwa kama binti huyo angepelekwa katika kituo cha
afya kama alivyoelekezwa na wahudumu wa Zahanati ya kijijini hapo
inayohudumia vijiji vitano vilivyopo katika kata hiyo na kata za
jirani. asingepoteza mtoto wake.

“Inashangaza kuona msichana huyo alipewa ushauri kwenda
kujifungua kituo cha afya Magoma lakini wazazi walipuuza ushauri huo
na kusababisha binti huyo kupoteza mtoto wake. Huo ni uzembe,” alisema
Mbunge huyo.

Mnzava aliwataka wnanachi kuzingatia maelekezo ya elimu ya afya
yanayoyotolewa na wataalam wa afya ili kuondoa matatizo na changamoto
mbalimbali zinazoweza kujitokeza.

Awali Mganga Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Vijijini, Miriam Cheche alisema
kuwa maeleze aliyopewa baada ya kufuatilia tatizo hilo aliambiwa na
binti huyo kuwa walipewa ushauri katika zahanati ya kijiji hicho wa
kwenda katika kituo cha afya cha Magoma kwa ajili ya kujifungus kwa
mujibu wa maelekezo ya kitaalamu .

Mganga huyo Mkuu alisema kuwa binti huyo alieleza kuwa Baba yake
alisisitiza apelekwe katika kituo cha afya lakini mama yake alikataa
na kusema kuwa atajifungulia nyumbani ambako alidai kuna wakunga
watakaomzalisha

“wangezingatia ushauri binti huyo asingetepoteza mtoto. Hata
angekwenda katika zahanati hiyo ya kijiji anageambiwa aende katika
kituo cha afya,” alisema Mganga Mkuu huyo.


Dk Miriam Cheche alisema kuwa hata hivyo Halmashauri hiyo inakabiliwa na
upungufu mkubwa wa watumishi wa afya ambayo inalazimika kusambaza
watumishi hao wawili kila zahanati.

Alieleza kuwa kuna vituo vya afya 49 ambavyo katika hivyo kuna
Hospitali moja na vituo na vituo vine vya afya. Alieleza sehemu za
huduma ya afya zitaongezeka kufikia 55 kutokana na kuwepo kwa maboma
6 ambayo yatakamilishwa kwa fedha zilizotolewa na serikali.


Kuhusu watumishi alisema kuwa sasa hivi wapo 270 na wameletewa wengine
43 ambao alisema bado ni kidogo kutokana na mahitaji. “Tunahitaji kuwa
na watumishi angalau 10 kila kituoa cha afya au zahanati ili kutoa
huduma ya kuridhisha.. aliwataka wananchi kuwa wavumilivu wakati
serikali inatatua tatizo la upungufu wa watumishi.

Mama mmoja Tatu Kasimu, Mkazi wa kijiji hicho aliiomba serikali iweke
kktuo cha afya hapo Kizara ili kuokoa kuondoa mateso ya wagonjwa ambao
wanalazimika kusafiti mwendo mrefu kwenda Magoma.

Mwingine Asia Abdalla Shewali Mhina alisema kuwa kila siku watu
wanapata elimu kuwa mimba ya kwanza wanataliwa kwenda katika kituoa
cha afya. “ Kila siku Tunapewa somo kuwa mimba ya kwanza nay a
kuendelea inabidi kwenda kuzalia katika kituoa cha afya. Kwa hiyo kama
ni kosa ni kosa lao wenyewe. Nesi hana kosa,” alisema.

Mbunge huyo ameanza ziara ya siku sita katika Jimbo lake Hilo.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...