Jeshi la Polisi Nchini limetoa onyo kwa baadhi ya madereva wa magari makubwa ya mazigo (malori) wanaohamasisha mgomo wa madereva ili kuzuia magari mengine yasifanye shughuli za usafirishaji kwa kisingizio cha madai ya haki zao wanazodai kutoka kwa waajiri wao kutokuwalipa posho zao na kufanya vitendo vya uvunjifu wa sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Kamishna wa Operesheni na Mafunzo CP Awadhi Juma Haji, amesema kuwa, Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa wanaotumia kisingizio cha mgomo huo kuzuia madereva wengine wasitoe huduma za usafirishaji na kuwataka wafuate taratibu za kisheria.

Aidha, kamishna Awadhi amewaagiza Makamanda wa Polisi wa mikoa kuwachukulia hatua kali za kisheria watu watakaobainika kuhamasisha madereva wenzao kufanya mgomo huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...