Na Mwandishi wetu, Babati


KADA maarufu wa Mjini Babati Mkoani Manyara, Emmanuel Khambay, amechukua fomu ya kuomba kupitishwa kugombea nafasi ya mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa kupitia Wilaya ya Babati Mjini.

Khambay amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa CCM wa Wilaya ya Babati Mjini Daniel Muhina, ambapo atagombea nafasi moja kati ya tatu zitakazogombewa ya mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa kupitia Wilaya ya Babati.

Khambay ambaye ni kada maarufu mjini Babati na Manyara kwa ujumla kutokana na kushiriki kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo, amethibitisha kuchukua fomu hiyo ila hakuwa tayari kuzungumza na vyombo vya habari kwa sasa.

Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya UVCCM Wilaya ya Babati Mjini, Idd Sulle amechukua fomu ya kuomba kugombea nafasi ya Katibu wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM mkoa wa Manyara.

Kada maarufu wa CCM mjini Babati, Cosmas Bura Masauda amejitosa na kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Babati Mjini.

Naye, Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la COSITA, Patrice Gwasima, amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Babati Mjini.

Wanachama na makada mbalimbali wa CCM wapo kwenye mchakato wa kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali ambapo hatua ya matawi imeshafanyika na kuendelea ngazi ya Kata, Wilaya, Mkoa na Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...