Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

MKUU wa mkoa wa Pwani,Abubakar Kunenge amewataka wananchi wa kata  ya Mbwawa kutafuta eneo jengine la kujenga kituo cha Afya  kutokana na eneo la Kwanza kutokidhi vigezo na masharti ya Serikali .

Aidha ametoa maelekezo kuwa kituo cha Afya cha awali kifanyiwe marekebisho  kwa kujenga wodi ya wazazi.

Kunenge pia ameagiza wananchi hao kutumia fedha  walizouza trekta Shillingi milion 9 kuanza ujenzi wa wodi ya wazazi katika  zahanati hiyo.

Agizo hilo amelitoa, wakati  wa mkutano  wa wananchi wa kata hiyo baada ya kutokea  mgogoro  wa ardhi  katika eneo la ujenzi wa kituo hicho.
 
Kunenge  amewaeleza wakazi wa Mbwawa kuwa, eneo  walilolichagua ambalo lina ukubwa wa hekari 6  ni ndogo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya, na kwa mujibu wa katiba ya nchi kituo cha Afya kinatakiwa kuwa na hekari 15.

"Utaratibu wa kujenga kituo cha Afya ni lazima eneo liwe na ukubwa wa hekari 15 "sasa eneo  hili no hekari 6  tu hivyo halitoshi badala yake nataka eneo hili mjenge wodi ya wazazi" alisema Kunenge.

Amewaeleza, wananchi  wa Mbwawa kutumia eneo  hilo kwaajili ya  ujenzi wa wodi ya wazazi na amewaruhusu kutumia fedha hizo Shilingi milioni tisa kuanza    ujenzi wa wodi ya wazazi na kusema serikali ya Mkoa kupitia Halmashauri itasaidia  kumalizia ujenzi huo.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mkuu wa Wilaya ya Pwani Bi. Sara Msafiri  alimueleza Mkuu wa mkoa  kuwa eneo hilo la Mbwawa linahitaji kuwa na kituo cha  Afya Kwani ni eneo lenye wananchi wengi na wanapata  changamoto ya  kufuata huduma za Afya katika kituo cha Mlandizi

Sara alieleza kuwa walishafanya utaratibu wa kutafuta eneo lingine la kujenga kituo cha Afya, badala  ya eneo la awali kutokukidhi vigezo.

 Aliendelea kusema  tayari serikari ya awamu ya sita  chini ya uongozi  wa Mama Samia imeshatoa  Shilingi Bilioni 2 kwaajili ya ujenzi wa  kituo cha Afya Cha kisasa kwani eneo hilo lina watu  wengi na wanahitaji huduma ya afya.

Sara pia alifafanua kuhusu  sintofahamu iliyojitokeza kuwa eneo la awali lenye ukubwa was hekari 6 Lina mgogoro  na kusema kuwa  eneo hilo ni Mali  halali ya serikari na halina mgogoro wowote.

 Aliendelea kusema Kama Kuna mtu anadai eneo ni lake basi aende Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na  nyaraka sahihi na taratibu za kisheria zitafatwa.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...