Njombe

WATU wanne wamenusuriko kifo mara baada ya bajaji namba MC 567 CJK aina ya TVS iliyokuwa ikitoka maeneo ya stendi kuu ya mji wa Njombe kuelekea katikati ya mji kupinduka kutokana na mlipuko mkubwa wa simu ya abiria uliosababisha moto.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Hamis Issah amesema bajaji hiyo imepinduka kutokana na dereva kugeuka nyuma kutokana na taharuki ya kulipuka kwa simu ndogo mali ya Siston Antony katika barabara kuu ya Njombe-Songea majira ya saa tano asubuhi.

“Moto umelipuka mkubwa na dereva wa bajaji akageuka kuangalia abiria wake na kushindwa kuiongoza akaiachia bajaji wakapinduka”amesema Kamanda Issah.

Kamanda Issah amesema baada ya ajali hiyo polisi imeweza kuingilia kati kutokana na mmiliki wa bajaji kutaka kulipwa na abiria mmiliki wa simu iliyosababisha mlipuko na kupelekea kupinduka kwa bajaji na kuharibika.

Aidha Kamanda Issa ametoa wito kwa wamiliki wa vyombo vya moto kuwa na bima za vyombo vyao ili kuepusha usumbufu kama huo huku pia akitoa rai kwa wamiliki wa simu kuwa makini na matumizi ya simu zao,na kubainisha kuwa abiria wote waliweza kupelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu ya majeraha madogo na kuruhusiwa kutoka ili kuendelea na shughuli zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...