Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo

WAKAZI wa Vitongoji vya Kata ya Kisutu, Jimbo la Bagamoyo ,Mkoa wa Pwani, wamemtaka mbunge wa Jimbo hilo Muharami Mkenge kuendelea kusimamia na kuzifikisha kero zao kwenye Mamlaka husika ili zipatiwe ufumbuzi ikiwa ni pamoja na kero ya umeme, maji , miundombinu mibovu ya barabara na fedha za Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF).
 
Wakitoa kilio cha changamoto hizo, wakati wa mkutano na mbunge huyo , baadhi ya wakazi akiwemo Farida Ramadhani,Matuka Mnyimadi  walisema shule imejengwa, Lakini bado wana kero ya barabara Na hawajasajiliwa kipindi kirefu wanachama wapya katika TASAF.

Chrisantus Joseph amemuomba mbunge kuingilia kati kero ya ushuru wa mafuta katika Bandari ya Bagamoyo.

Akizungumza na wakazi hao , Muharami Mkenge alieleza, Serikali inaendelea na juhudi za kuwapatia maendeleo wananchi wake kwa awamu .

Aliwaomba wananchi kuvuta subira wakati Serikali ikiendelea kutatua kero za maji, barabara na umeme kwenye Maeneo ambayo bado hayajafikiwa.

"Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu imetekeleza mengi kwenye sekta na nyanja mbalimbali ya maji, barabara za mijini na Vijijini,umeme ambapo inaendelea kuongeza kutenga fedha nyingi hususan bajeti mpya ya 2022/2023 ili kutatua kero zilizopo".

Aidha Mkenge amezungumzia mradi mkubwa wa barabara unaotarajia kutekelezwa ambapo, sisi Bagamoyo tumeomba tujengewe barabara ndani ya mji, mifereji, lambo na mambo mbalimbali," alisema Mkenge.

Mkenge pia aliwasihi wananchi kujitokeza katika Zoezi la sensa agost 23 mwaka huu kila mmoja ashiriki bila kukosa,kwani itasaidia kuweka mipango mizuri ya kimaendeleo kwa kuwa na idadi kamili ya watu na makazi.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...