Na John Walter-Babati

Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Daniel Sillo ametoa mabati 600 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miradi ya elimu na afya jimboni humo.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo agosti 26,2022 katika ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Babati ikiwa ni mkakati wa Mbunge huyo (CCM) kusaidia kukamilisha miradi ya afya na elimu inayoendelea kujengwa wilayani hapo.

Mbunge huyo ametoa mabati hayo kwa mgawanyo katika vijiji sita vya Tsamas (150), ,Secheda (117),Boay (84),Kisangaji (29),Datar (110) na Yorotonik (110).

Amewataka madiwani na watendaji wengine kusimamia bati hizo zikatumike kwenye miradi iliyokusudiwa.

Aidha ameishukuru benki ya NMB kwa msaada huo walioutoa ambao umetokana na mahusiano mazuri waliyonayo yeye na benki hiyo.

Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Babati imempongeza Mbunge Sillo kwa jitihada za kuwaletea wananchi maendeleo kama inavyoelekeza ilani ya chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza kwa niaba ya madiwani, diwani wa kata ya Ufana Bernad Bajuta amesema mabati hayo yatasaidia sana kumaliza miradi ya elimu na afya iliyokwama kwa muda mrefu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...