Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amezindua rasmi Programu ya mafunzo yanayolenga kuImarisha huduma kwa wadau walio katika mnyororo wa huduma za Utalii inayoendeshwa na Chuo Cha Taifa cha Utalii (NCT) nchini.

Programu hiyo iliyozinduliwa leo na kufadhiliwa na Bank ya NMB inawahusu maafisa uhamiaji kama wadau muhimu watakaofaidika na mafunzo hayo katika mikoa yenye malango makuu ya kuingilia watalii nchini yaani Dar es salaam, Zanzibar na Arusha na Kilimanjaro ambapo takribani maafisa 700 wa uhamiaji watanufaika na programu hiyo.

Licha ya kuishukuru Benki ya NMB kwa mchango wake mkubwa, Waziri Mhe.Balozi Dkt.Pindi Chana ametoa wito kwa wadau wengine wa Utalii kujitokeza kuunga Mkono Juhudi za Serikali chini ya Mhe Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za kuendeleza sekta ya Utalii kwa maslai mapana ya watanzania wote

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Chuo Cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt.Shogo Mlozi, amesema wanakusudia kuwafikia wadau zaidi ya 5,000 kutoka Dar es Salaam, Zanzibar, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Mara na mikoa mingine ya Tanzania kwa kuwa maeneo hayo yanahuduma nyingi za Kitalii.
 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...