Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Wakuu wa Vikosi wakiwa kwenye picha ya pamoja na Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu CP Benedict Wakulyamba (katikati) ambapo kwa pamoja walitembelea hifadhi ya taifa ya Mikumi na kujionea utalii na vivutio vilivyopo kwenye hifadhi hiyo. Kamishna Wakulyamba pia aliwataka wananchi kuendelea kulinda rasilimali za utalii na kutembelea utalii wa ndani. Picha na Demetrius Njimbwi Jeshi la Polisi
23 OKTOBA 2022 MIKUMI, MOROGORO
Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Wakuu wa Vikosi wamewaonya baadhi ya watu wanaofanya vitendo vya ujagili na kuharibu baadhi ya vivutio mbalimbali vya taifa ambavyo ni urithi wa vizazi vijavyo.
Akiwaongoza kutembelea hifadhi ya taifa ya Mikumi, kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu CP Benedict Wakulyamba amesema kuwa, kufuatia uzinduzi wa filamu ya Royal Tour imesaidia kufunguka kwa utalii nchini ambapo watu mbalimbali wamekuwa wakitembelea hifadhi pamoja na vivutio vilivyopo.
Aidha, kamishna Wakulyamba, amewataka wananchi na Watanzania kwa ujumla kuendelea kulinda rasilimalia za taifa pamoja na kutembelea na kufanya utalii wa ndani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...