Na.Khadija Seif, Michuzi Tv 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika hafla ya kutangaza matokea ya Sensa ya watu na Makazi mwishoni mwa mwezi Oktoba  mwaka huu.

Akizungumza Jijini Dar es salaam leo Oktoba 12,2022  Kamisaa wa Sensa Anna Makinda amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikamilisha rasmi zoezi la kuhesabu watu,Majengo pamoja na Anwani za Makazi kutokana na hamasa ya wananchi ambayo wameionyesha na kukamilisha zoezi hilo Kwa wepesi.

Makinda amefafanua zaidi kuwa Sensa ya mwaka huu imetumia teknolojia ya Hali ya juu iliyohusisha matumizi ya vishikwambi katika awamu zote za utekelezaji na kuongeza ubora wa takwimu zilizokusanywa.

"Tangu kukamilika Kwa zoezi la kuhesabu watu,wataalamu wamekuwa wakiendelea na kazi ya Uchakataji wa taarifa zilizokusanywa Ili kupata matokea mbalimbali ya sensa hiyo."

Aidha,Kamisaa ameeleza kuwa Serikali inatoa pongezi na kuwashukuru wananchi wote kwa namna walivyojitoa kuhakikisha Sensa ya watu na Makazi Kwa mwaka huu linafanikiwa.

"Serikali itaendelea kuwahusisha wanahabari katika kuelimisha na kuhamasisha umma kuhusu matumizi ya matokea ya sensa katika mipango jumuishi Kwa Maendeleo endelevu ya Taifa."

Kamisaa wa zoezi la Sensa Anna Makinda akizungumza na waandishi wahabari Leo Jijini Dar es salaam katika ofisi za takwimu na kutangaza rasmi kuwa Mgeni rasmi wa uzinduzi wa matokea ya Sensa anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan uzinduzi ambao utafanyika mwishoni mwa mwezi octoba mwaka huu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...