Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kabla hajaondoka nchini Oktoba 23, 2022, kwenda Korea ya Kusini kwa ziara ya kikazi. Kulia ni Mkewe Mary Majaliwa, wa pili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Heri James na wa tatu kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kabla hajaondoka nchini Oktoba 23, 2022, kwenda Korea ya Kusini kwa ziara ya kikazi. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Heri James na wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kabla hajaondoka nchini Oktoba 23, 2022, kwenda Korea ya Kusini kwa ziara ya kikazi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

*****************

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameondoka nchini leo (Jumapili, Oktoba 23, 2022) kwenda Seoul, Jamhuri ya Korea kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.

Akiwa Korea Kusini, Mheshimiwa Majaliwa atakutana na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mheshimiwa Han Duck-soo. Pia anatarajiwa kushiriki kongamano la biashara na kukutana na wamiliki wa makampuni makubwa na wenye viwanda. Vilevile, atakutana na Watanzania waishio Korea Kusini.

Kupitia vikao hivyo, Tanzania inatarajiwa kuimarisha mahusiano na Korea Kusini ambayo yamedumu kwa miaka 30. Vilevile, kukuza mahusiano ya kibiashara na uwekezaji, kuangalia fursa za kukuza uchumi wa bluu, utalii, mahusiano ya anga na ushirikiano kwenye sekta ya sanaa na utamaduni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...